Back
Ivory Coast: Makamu wa Rais ajiuzulu baada ya kifo cha waziri Mkuu
Jul 14, 2020
Siku chache baada ya kifo cha ghafla cha Waziri Mkuu wa Ivory Coast, Amadou Gon Coulibaly, Makamu wa Rais wa nchi hiyo Daniel Kablan Duncan amejiuzulu.
Imeelezwa kuwa, Makamu huyo anaachia nafasi kutokana na sababu binafsi na kwamba aliwasilisha barua ya kujiuzulu kwa mara ya kwanza mwezi Februari.
Kifo cha ghafla cha Coulibaly ambaye alikuwa chaguo la Rais Alassane Ouattara kurithi kiti cha Urais kimepelekea Chama tawala kuanza kutafuta upya Mgombea, mchakato ambao Wachambuzi wamesema unaweza kusababisha mvutano.
Kufuatia kifo cha Coulibaly aliyekuwa akisumbuliwa na matatizo ya moyo kwa muda mrefu, Chama tawala cha RHDP kimesema kinaweza kumuomba Rais kufikiria kuongeza muda.
comments
0Shares
0Comments
0Favorites
1Likes
Say something to impress...
Loading...
Comments
Hot

No content at this moment.

Relevant people
Mseto
18580 Followers
Taarifa kwa utendeti
Related