Back
Eymael: Simba Tulieni Dozi Yenu Ipo Tayari
Jul 4, 2020
KOCHA Mkuu wa Yanga, Mbelgiji, Luc Eymael ameibuka na kusema kuwa hana presha na Simba kuwafuata katika Hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la FA kwa kuwa tayari ameshawaandalia dawa.
Mbelgiji huyo ametoa kauli hiyo muda mchache baada ya Simba kuifunga Azam FC mabao 2-0 katika mchezo wa Kombe la FA uliopigwa juzi Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar ambapo nusu fainali ya wababe hao inatarajiwa kupigwa Julai 12, mwaka huu.
“Sina presha juu ya Simba kuingia hatua ya nusu fainali kwa sababu kila kitu kwetu kipo sawa kwa sababu nahitaji kuendeleza rekodi dhidi yao, najua mechi kubwa ambayo imekuwa ikivuta hisia za wengi lakini hata wachezaji wenyewe wamefurahi na wanashukuru kwamba tunaenda kucheza na Simba kwenye hatua hiyo,” alisema Eymael.
Stori: Ibrahim Mussa, Dar es Salaam
0Shares
0Comments
0Favorites
0Likes
Say something to impress...
Loading...
Comments
Hot

No content at this moment.

Relevant people
Mseto
18580 Followers
Taarifa kwa utendeti
Related