Back
Upinzani washinda Urais Malawi
Jun 28, 2020
Spread the love
LAZARUS Chakwera, Kiongozi wa upinzani nchini Malawi, ameibuka mshindi wa Urais katika uchaguzi wa marudio nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu kwa msaada wa mashirika ya kimataifa…(endelea).
Tume ya Uchaguzi Malawi (MEC) imesema, Chakwera amemshinda Rais aliyepo madarakani, Peter Mutharika kwa asilimia 58.57.
Uchaguzi huo umefanyika Jumanne iliyopita tarehe 23 Juni 2020 baada ya ule wa awali, uliofanyika Mei 2019 kufutwa na Mahakama nchini humo Februari 2020 kutokana na kubainika ulitawaliwa na dosari.
Katika uchaguzi huo wa Mei 2019, Rais Mutharika aliibuka mshindi kwa kupata asilimia 38.57 huku Chakwera akipata asilimia 35.41.
Hata hivyo, Chakwera hakukubali matokeo hayo na kuamua kufungua kesi mahakamani kuyapinga na Februari 2020 akashinda kesi hiyo na uchaguzi ukarudiwa na yeye kuibuka mshindi.
Baada uamuzi huo wa Mahakama, Rais Mutharika alikwenda mahakama ya rufaa kupinga uamuzi huo ambapo hakufanikiwa kushinda.
Kilichotokea Malawi kufutwa kwa matokeo kinafanana na kile kilichofanywa na Mahakama ya Juu nchini Kenya mwaka 2017 kufuta matokeo yaliyokuwa yamempa ushindi Rais Uhuru Kenyatta.
Hata hivyo, uchaguzi wa marudio ulipofanya, mgombea wa upinzani, Raila Odinga aliyefungua kesi hiyo hakushiriki na Rais Kenyatta kuibuka mshindi katika uchaguzi ambao haukuwa na upinzani mkali.
14Shares
0Comments
0Favorites
5Likes
Say something to impress...
Loading...
Comments
Hot

No content at this moment.

Relevant people
Matukio Kimapenzi!
5504 Followers
Matukio Kimapenzi! Kimapenzi, Kingono zaidi zaidi!
Related